Tuesday 29 May 2018

JINSI YA KUPATA MKOPO

Shalom vicoba group imekuwa ikitoa mikopo na kusajili wanachama wapya toka mwaka 2016. Shalom vicoba group iliendelea kufanya kazi Kama kikundi cha kukopeshana na kufikia mwaka 2019 mwezi wa nne ilisajiliwa rasmi Kama Saccos.
Saccos hiyo iliitwa shalom saccos Limited na kupata usajili namba SIR/733.
Ili uweze kupata mkopo unao hitaji lazima uwe na vigezo vifuatavyo:-
  1. Uwe umejiunga kwenye shalom vicoba group na kulipia kiingilio cha Tshs. 30,000/=
  2. Uwe umenunua HISA za msingi 20 ambapo kila Hisa huuzwa kwa Tshs 10,000/= na Jumla kupelekea Tshs. 200,000/=
  3. Uwe mtendakazi kwenye makanisa yenye ushirika wenza na shirika la Compassion International Tanzania.
  4. Uwe na mkataba wa kazi wa sasa.
  5. Uwe na AKIBA itakayokuwezesha kukopa mara tatu ya kiwango unachohitaji. Mfano unataka kukopa milioni tatu, basi LAZIMA uwe na AKIBA ya Tshs. 1,000,000/=

VIAMBATANISHO WAKATI WA KUCHUKUA MKOPO.
  1.  Fomu ya mkopo ambayo inapatikana kwa Tshs. 10,000/= tu.
  2. Mkataba wa ajira
  3. salary slip tatu za hivi karibuni zilizosainiwa na mwajiri na kuwekwa Muhuri.
  4. standing order ya Benki

No comments:

Post a Comment